SOKO LA MTANDAO TANZANIA Jisajili na kuweka Matangazo BURE MILELE! 0677775000
classiera loader
image

Ad Details

  • Ad ID: 16199

  • Added: 28th December 2022

  • Sale Price: TZS1

  • Location: Tanzania

  • State: Arusha Region

  • Phone: +255684450076

  • Views: 138

Description

*Kufika Kileleni Mapema: Takwimu & Sababu Zake*

Tendo la ndoa linapaswa kudumu kwa dakika ngapi?

Hili ni swali maarufu sana mtaani ambalo pengine hata wewe umewahi kujiuliza.

Kwa mujibu wa utafiti, muda wa kawaida wa kushiriki tendo la ndoa ni dakika 7-13.

Dakika 1-6 ni muda mchache sana na zaidi ya dakika 13 ni muda mrefu

Kwa mantiki hii, tutatumia muda wa dakika 1-6 kama muda mchache unao ashiria tatizo la kuwahi kufika kileleni.

Ni muhimu kukumbusha kuwa, muda uliotajwa kwenye utafiti huu hauhusishi michezo ya kabla ya tendo la ndoa pamoja na mambo mengine yanayo fanyika kabla ya tendo husika.

Ni muda ambao uume hupaswa kuwa ndani ya uke kabla ya kufika kileleni.

*Takwimu*
Inakadiriwa kuwa asilimia 30 ya idadi ya wanaume wote duniani wanakabiliwa na tatizo hili.

Hii ina maanisha kuwa, katika kila kundi la wanaume 100, 30 kati yao huwa na tatizo la kuwahi kufika kileleni.

Wanaume hawa huwa hawawezi kushiriki tendo la ndoa kwa muda mrefu.

Baada tu ya kuingiza uume kwenye uke, msisimko wa kihisia huwa mkubwa kwa kiwango ambacho huwafanya washindwe kujizuia kufika kileleni mapema.

Jambo hili hutokea pasipo wao kupenda, na husababishwa na mambo ambayo tunaweza kuyagawa kwenye makundi matatu;

Sababu za kimaumbile
Sababu za kisaikolojia na kihisia
Sababu za kibaiolojia
Tutaelezea sababu zote hizi kwa ujumla wake kama ifuatavyo;

Sababu Za Kimaumbile
1. Msisimko Mkubwa
Baadhi ya wanaume huwa na uume wenye msisimko mkubwa sana wa kihisia.

Tatizo hili linaweza kuwa la kuzaliwa, wengine hulipata kwenye kipindi fulani cha maisha yao.

Watu hawa huwa hawawezi kujizuia kumwaga shahawa kwa kuwa baada tu ya uume kukutana na uke, msisimko mkubwa hutokea.

Kama unawahi sana kufika kileleni, pengine wewe pia una tatizo hili.

Sababu Za Kisaikolojia Na Hisia
1. Uoga Na Wasiwasi
Unaweza kusababishwa na penzi jipya, kukosa kujiamini, kutazama video za ngono, kutokushiriki tendo hili mara kwa mara, majuto, kutazama ponografia au kuwa na furaha kubwa kupita kiasi kutokana sababu mbalimbali.

Jaribu kuwaza majuto ya dhamiri anayoweza kuwa nayo mwanamme mwenye kufanya mapenzi na mwanamke mpya huku wakiwa kwenye ndoa au uhusiano na mwanamke mwingine ambaye wanapendana sana.

Tazama mfano mwingine. Jaribu kuwaza siku ambayo mwanamme mwenye haiba ya kawaida anapokutana kimwili na mwanamke anayetazamwa na jamii kama mtu mwenye ushawishi mkubwa, au maarufu.

Uwezekano wa kushindwa kabisa kushiriki tendo la ndoa, au kuwahi sana kufika kileleni ni mkubwa.

Yapo mazingira mengi yanayoleta wasiwasi na uoga wa kushiriki tendo la ndoa.

Vyote hivi vinaweza kuwa sababu ya kufika kileleni mapema.

2. Mkazo
Neno hili linaweza kukufanya usielewe. Lina maana sawa na stress.

Mkazo ni jibu la mwili linalotolewa kutokana na uwepo wa aina fulani la shinikizo la kimazingira, kiakili au kimwili.

Mfano wa sababu zinazoweza kusababisha mtu awe na stress ni mapambano ya kiuchumi, ukosefu wa ajira, matatizo ya kifamilia au uwepo wa changamoto kadhaa kwenye eneo la kazi.

Katika mazingira ya stress, mwili huzalisha kiasi kikubwa cha vichocheo vya cortisol na epinephrine ambavyo huuandaa kuikabili changamoto husika kupambana au kukimbia.

Huongeza wasiwasi, mapigo ya moyo na shinikizo la damu pamoja na kupunguza uzalishwaji wa vichocheo vya kiume pamoja na hamu ya kushiriki tendo la ndoa.

Athari zke zinaweza kujidhihirisha kwenye ufanisi wa kushiriki tendo la ndoa.

3. Sonona
Kwa mujibu wa WHO, watu milioni 280 duniani ni wagonjwa wa sonona, na zaidi ya watu 700,000 hujiua kila mwaka kutokana na tatizo hili.

Huu ni ugonjwa wa akili unaomfanya mhusika ajihisi yupo peke yake, mnyonge, hathaminiwi na jamii na wala maisha hana maana yoyote duniani.

Watu hawa hujiona wakosefu, hupoteza hamu ya kila jambo na huona kujiua ndiyo jawabu pekee la kuondokana na changamoto za kidunia.

Tatizo hili huwa na uhusiano mkubwa sana na changamoto ya kufika kileleni mapema.

4. Kumbukumbu Mbaya
Tafiti za afya zinasema kuwa walau mwanamme mmoja katika kila kundi la wanaume watatu kwenye kipindi fulani cha maisha yake aliwahi kupatwa na changamoto ya kuwahi kufika kileleni.

Tendo hili hupunguza kujiamini, na humfanya mwanaume husika ajione dhaifu.

Aidha, ukomavu mkubwa wa kisaikolojia huhitajika ili kufuta kumbukumbu hii mbaya ambayo ikiachwa inaweza kuwa chanzo cha muendelezo wa kutokea kwa tatizo husika.

Kuendelea kukumbuka tukio hili baya hufanya tatizo liwe kubwa zaidi, lakini kukubali uwepo wake na kujipa nafasi ya pili hulitibu na kufanya liondoke kabisa.

5. Changamoto Za Mahusiano
Baadhi ya wanaume huwa na uwezo mzuri tu wa kushiriki tendo la ndoa pasipo uwepo wa tatizo lolote.

Changamoto huanza kutokea baada ya kuvunjika kwa uhusiano huo na kuhamia kwa mwanamke mwingine ambaye tabia zake huwa tofauti na zile za mwanamke wa mwanzo.

Chukulia mfano, uhusiano wenye migogoro ya mara kwa mara, au ule ambao mwanamme huwa hapewi tendo la ndoa kwa kadri ya uhitaji wake.

Mambo haya yanaweza kuwa sababu ya mwanamme kufika kileleni mapema kwa sababu humfanya ashiriki tendo la ndoa pasipo kuwa na uhuru.

*Sababu Za Kibaiolojia*
Baadhi ya wanaume hurithi tabia fulani kutoka kwa wazazi wao ambazo huwa na uhusiano wa moja kwa moja na tatizo la kuwahi kufika kileleni.

Mpangilio wa vinasaba karibu na jini za SIM 1 huhusishwa na ongezeko la zaidi ya asilimia 26 ya tatizo la upungufu wa nguvu za kiume, kuwahi kufika kileleni ikiwemo.

Mvurugiko wa vichocheo vya oxytocin, luteinizing hormone (LH), prolactin na thyroid stimulating hormone (TSH) unaweza kuwa chanzo cha kutokea kwa tatizo hili.

Aidha, uchache wa kemikali za serotonin na dopamine ambazo huhusika na muamsho wa kihisia kwenye ubongo inaweza pia kuwa sababu ya kutokea kwake.

*NYONGEZA*
Kuna pointi mbili hazijatajwa kwenye makala hii, najua unawaza sana kuwa imewezekanaje zisiwe miongoni mwa sababu za tatizo la kuwahi kufika kileleni.

Upungufu wa nguvu za kiume na kufanya punyeto, au kwa lugha ya staha kidogo kujichua.

Kuwahi kufika kileleni kunaweza pia kuhusishwa na uwepo wa tatizo kubwa la upungufu wa nguvu za kiume.

Hata hivyo, ifahamike kuwa, siyo kila mwanamme anayewahi kufika kileleni anakuwa na changamoto ya upungufu wa nguvu za kiume.

Ni wanaume wachache sana ambao huwahi kufika kileleni huwa na upungufu za nguvu za kiume.

Kuhusu punyeto, hakuna ushahidi wa wazi wa kisayansi unaothibitisha kuwa kitendo hiki humfanya mhusika apatwe na changamoto ya kuwahi kufika kileleni.

Badala yake, ni tendo ambalo katika nyakati fulani hutumika kutibu changamoto za watu wanaowahi kufika kileleni.

Hakuna uhusiano wa moja kwa moja kati ya kujichua na kuwahi kufika kileleni.

Hata hivyo, kila jambo linapofanyika kwa kiasi kikubwa pasipo udhibiti huleta athari kwa afya.

Hivyo, ni lazima pia tendo hili lifanyike kwa kiasi na tahadhari kubwa.

*Hitimisho*
Baadhi ya magonjwa sugu hasa kisukari na shinikizo la juu la damu yanaweza pia kuwa chanzo cha kutokea kwa changamoto hii.

Ni muhimu kufanya uchunguzi wa afya ili kubaini chanzo halisi inayofanya litokee.

Baada ya kupitia kipindi kigumu cha kuwahi kufika kileleni, bado unayo nafasi ya pili katika kurejesha heshima ya ndoa.—

USIULIZE SWALI’ BALI NI WAKATI WAKO SAHIHI KUANZA DOZI YA KUIMALISHA VICHO’CHEO KABRA JAMA ZAKO HAWA JAMUFIKISHA KILELENI MMKEO

Tags :

Bids

BID Stats : 0  Bids posted on this ad

Let’s Create Your Bid

Only registered user can post offer *

Ad Price

TZS1

classiera loader

Related ads

LIST YOUR BUSINESS TODAY!!